Sikomi

Sikomi
By Diamond Platnumz

Wanasemaga mapenzi safari
Unavyopita ndo jinsi unajongea
Ila niendako ni mbali sijui ka ntafika sababu natembea
Niliposikiaga Habari
Yakisifika nikakesha nangojea ah
Akabariki jalali na nikawika muziki nikauotea
Ile pruu mpaka Macca
Nikadandiaga Bongo movie
Kumbe mapenzi hayataki haraka
Ni kama tango natia tu chumvi
Mwenzenu nikaoza haswa
Na kujitia kitandani mjuzi
Eti nataka fukuza paka
Badala ya mbwa nikafuga mbuzi
Uhmm
Wivu ukanifanya nikagombana na ma rafiki
Ugomvi na mamangu akiniambia siambiliki

Moyo ukanambia Nasibu sasa mapenzi basi
Ila nang’ang’ania najaribu kuipinga nafsi
Esma ananiambia mdogo wangu mapenzi basi
Ila nang’ang’ania
Nikiumizwa na huyu kesho nna mwingine

[Chorus:] Ooh mbona sikomi
Sikomi
Sikomi
Licha ya mateso haya
Najiuliza (oh sikomi)
Oh sikomi mbona (sikomi)
Mbona jamani
Sikomi
Licha ya mateso haya ah
Uhmm

Aliyonifania wa central
Haki ya mungu siyawezi sema
Ila nimejifunza kesho nisiwaamini wacheza sinema
Moyo walinipatia mateso
Siwezi kumeza siwezi tema
Ndiyo maana sikushanga ile ghafla
Toka CCM kwenda Chadema
Wanasema kitanda ukitandika sharti ukilalie
Nikajitia ukamanda yatakwisha
Wacha nivumilie
Kila kiza kikitanda
Ndo visa machozi me nilie
Penzi yakatia parapanda
Kuwaita waje washambulie
Acha na penny we darling
Niliyo muhongaga gari aliponambia ana mimba
Mwisho wa siku akaichomowa (chali)
Mola akanitunuku zari
Akanzaliya dume na mwali
Niliyvo mjinga nika cheat aibu mpaka
Kwa vyombo vya habari

Moyo unanambia Nasibu sasa mapenzi basi
Ila nang’ang’ania najaribu kuipinga nafsi
Laizer ananiambia simba mapenzi basi
Ila nang’ang’ania
Nikiumizwa na huyu kesho nna mwingine

Chorus

Mateso mama
Ayo Laizer